Monday, July 27, 2015

Ujuwe Umbali wa wastani baina ya mwezi na dunia..



Picha maarufu sana ya dunia yetu iliyopigwa na Mwanaanga Kutoka Marekani Bill Anders wakati wa ujumbe wa Apollo 8.
Tarehe 24 Desemba 1968. Apollo 8 ilikuwa mara ya kwanza chombo cha angani cha kubebea watu kushikwa na graviti ya mwezi na kuzunguka mwezi kwa ajili ya gravity hiyo.
Picha inayoonyesha umbali baina ya dunia na mwezi kulingana na ukubwa wao.
Umbali wa wastani baina ya mwezi na dunia ni kilomita 384,400. Mwezi wetu una upana wa kilomita 3,470. Dunia yetu ina upana wa kilomita 12,800

Wednesday, July 22, 2015

Zilikuwa zama za Ubaguzi wa Rangi Kwenye Mauaji ya Sharpeville

Ilikuwa ni tarehe 28,Mei1960 Afrika Kusini Mjini Sharvpeville Ambapo Polisi Africa Kusini waliwauwa wanachi wenye Rangi Nyeusi wapatao 69....

Leo nina historia ya Jane Matlida Bolin

Mwanamke mwenye Historia yake nchini marekani Jane M Bolin alizaliwa April 11,1908 January 8,2007 Alifariki.
1939 Jane M Bolin alikuwa mwanamke wa kwanza mweusi kuwa jaji katika Mahakama Kuu ya Marekani......

Tuesday, July 7, 2015

Tazama Picha Kadha zikionyesha Ukaribu wa Sokwe na Jane Goodall....


Msichana kutoka wingereza Jane Morris Goodall alisafiri kutoka Wingereza Mpaka kigoma Tanzania mwambao mwaziwa Tanganyika,
Mwaka 1960 alikuwa ana Umri wa miaka 26 tu!! Lakini Ali shangaza ulimwengu kwa kazi yake ya Primatology (Elimu ya wanyama na Mimea) Aliyo Ifanya katika hifadhi ya Msitu wa Gombe Mpaka sasa hifadhi ina Sokwe zaidi ya 700..
Nimengi amefanya lakini kubwa zaidi ni 1977 aliamuwa kanzisha Chuo Cha Jane Goodall Institute for Wildlife Research



Uhaba wa Madarasa Maili Kumi Mtwara...

Wanafunzi wa shule ya msingi Mail Kumi iliyopo halmashauri ya Mtwara vijijini wanalazimika kusoma katika mazingira mabovu kutokana na bajeti ya fedha iliyotakiwa kuongeza madarasa  katika shule hiyo kupelekwa kwenye ujenzi wa maabara.
 Mkuu wa shule hiyo Mussa Mshangani anasema shule hiyo ina mikondo minne na inawanafuzi 223 huku madarasa yakiwa mawili tu hali inayowalazimu baadhi yao kusoma katika madarasa ya mbavu za mbwa. 
Akizungumzia changamoto hiyo kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Mtwara vijijini Oscar Ng’itu anasema lengo la halmashauri ni kuongeza madarasa lakini hilo limeshindikana kutokana na sehemu kubwa ya vyanzo vya mapato kupelekwa  kwenye ujenzi wa maabara.
  Hata hivyo mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho saidi mchomeko anasema umasikini lakini pia muitikio duni wa elimu katika kijiji cha maili kumi unachangia wananchi kushindwa kujitolea ipasavyo katika ujenzi wa madarasa.

Mtandao usiokubali dhambi wavutia wengi...

Waanzilishi wa Facegloria wanadai kwamba mtandao huo umewavutia wafuasi takriban laki moja tangu uzinduliwe mwezi Juni.
Kuna maneno 600 yaliopigwa marufuku katika mtandao huo na kuna kibonyezo cha "Amen" kushabikia ujumbe unaobandikwa.
Ummaland, ni mtandao wa kijamii wa kiislamu uliozinduliwa 2013, can una wafuasi 329,000.
Unatoa fursa kwa wanawake kuwa na faragha zaidi na kutoa ujumbe wa nasaha wa kidini kila siku.


Sura ya Facegloria haitofautiani sana na Facebook

Joto Uingereza lilifika Degrees 36 za Centigrade

Story kutoka Uingereza inahusu record ya juu ya joto ambayo haijawahi kutokea kwa kipindi cha kama miaka 10 hivi.
Kiwango cha joto imefikia degrees 36 za Centigrade..




 Kiwango hiki cha joto mara ya mwisho kilirekodiwa mwaka 2006, July 1 2015 imetokea tena.. Pichaz Kadha zinazoonesha hali ilivyo maeneo mbalimbali.......

Zimbabwe Yauza Tembo wake China...

Zimbabwe inasema inahitaji fedha kukabiliana na uwindaji haramu, lakini mashirika ya kutetea maslahi ya wanyama yameghadhabishwa na hatua hiyo.Waziri wa mazingira Zimbabwe amesema tembo hao walisafirishwa kwa ndege hadi China kwenye ndege binafsi ya mizigo.Wahifadhi wanyama wanasema tembo wanahitaji uangalifu wa miaka kadhaa kutoka kwa wazazi wake na kwahivyo kuwatenganisha tembo hao wadogo kutoka jamii zao katika umri mdogo ni kitendo cha ukatili na kitakacho kuwa na athari kubwa kwa wanyama hao...

Monday, July 6, 2015

Unaambiwa kuna visiwa zaidi ya 2500 Katika Bahari ya Pasifiki...

Pasifiki inayoonekana kutoka angani; 
Pasifiki ni bahari kubwa kuliko bahari zote duniani.Iko kati ya Bara la Amerika kwa upande wa mashariki na Bara la Asia / Australia upanda wa magharibi. Eneo lake ni karibu nusu ya uso wa dunia. Eneo lake ni kilometa za mraba milioni 179.7 ambayo si bahari kubwa tu bali pia ni eneo kubwa kuliko nchi kavu yote duniani. Visiwa vyake vingi huhesabiwa mara nyingi pamoja na Australia kama "Australia na Pasifiki".Pasifiki ina kina cha wastani wa mita 4,028; kina kikubwa katika mfereji wa Mariana kinafikia mita 11,034.
Kuna visiwa zaidi ya 25,000 katika Pasifiki vingi ni vidogo sana.....

Thursday, July 2, 2015

Tazama hii ujuwe ukali wa Tanzani Zanzibar


Melia Zanzibar

Ijuwe Hifadhi ya Gombe Kigoma


Hifadhi ya Taifa  ya GOMBE ni hifadhi iliyoanzishwa  maalumu kwa ajili  ya  tafiti  za Kisayansi  hususani  katika kuwalinda  na kuwahifadhi Wanyamapori adimu  wa jamii  ya Sokwe mtu  (chimpanzees) ambao wapo  hatarini   kutoweka  duniani (Endangered species). 
Hifadhi  hii ya Gombe  ilianzishwa  rasmi mwaka 1968 mkoani  Kigoma  katika  mwambao  wa ziwa Tanganyika, upande  wa mashariki  takribani  umbali wa kilomita  24  kwa njia ya usafiri wa maji ya Ziwa Tanganyika Kaskazini mwa Mji wa  Kigoma. 
Hifadhi   hii imegawanyishwa katika kanda  4  ambazo  ni pamoja  na kanda za fukwe , kanda za ziwa,  kanda za maeneo  ya mapori, msitu  na utawala wa hifadhi.

Usafiri wa Boti hutumika Zaidi kwa Watu wanao Safiri Kuelekea katika Hifadhi ya Gombe