Thursday, July 2, 2015

Ijuwe Hifadhi ya Gombe Kigoma


Hifadhi ya Taifa  ya GOMBE ni hifadhi iliyoanzishwa  maalumu kwa ajili  ya  tafiti  za Kisayansi  hususani  katika kuwalinda  na kuwahifadhi Wanyamapori adimu  wa jamii  ya Sokwe mtu  (chimpanzees) ambao wapo  hatarini   kutoweka  duniani (Endangered species). 
Hifadhi  hii ya Gombe  ilianzishwa  rasmi mwaka 1968 mkoani  Kigoma  katika  mwambao  wa ziwa Tanganyika, upande  wa mashariki  takribani  umbali wa kilomita  24  kwa njia ya usafiri wa maji ya Ziwa Tanganyika Kaskazini mwa Mji wa  Kigoma. 
Hifadhi   hii imegawanyishwa katika kanda  4  ambazo  ni pamoja  na kanda za fukwe , kanda za ziwa,  kanda za maeneo  ya mapori, msitu  na utawala wa hifadhi.

Usafiri wa Boti hutumika Zaidi kwa Watu wanao Safiri Kuelekea katika Hifadhi ya Gombe

Maporomoko ya maji  ya Kalambo  vile vile  hutirirka  na kuingia  katika  hifadhi  za taifa  za  Gombe



Huu ni Ufukwe wa Ziwa Tanganyika katika Hifadhi ya Gombe