Tuesday, July 7, 2015

Uhaba wa Madarasa Maili Kumi Mtwara...

Wanafunzi wa shule ya msingi Mail Kumi iliyopo halmashauri ya Mtwara vijijini wanalazimika kusoma katika mazingira mabovu kutokana na bajeti ya fedha iliyotakiwa kuongeza madarasa  katika shule hiyo kupelekwa kwenye ujenzi wa maabara.
 Mkuu wa shule hiyo Mussa Mshangani anasema shule hiyo ina mikondo minne na inawanafuzi 223 huku madarasa yakiwa mawili tu hali inayowalazimu baadhi yao kusoma katika madarasa ya mbavu za mbwa. 
Akizungumzia changamoto hiyo kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Mtwara vijijini Oscar Ng’itu anasema lengo la halmashauri ni kuongeza madarasa lakini hilo limeshindikana kutokana na sehemu kubwa ya vyanzo vya mapato kupelekwa  kwenye ujenzi wa maabara.
  Hata hivyo mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho saidi mchomeko anasema umasikini lakini pia muitikio duni wa elimu katika kijiji cha maili kumi unachangia wananchi kushindwa kujitolea ipasavyo katika ujenzi wa madarasa.