Idadi
kubwa ya watu linapokuja suala la pesa, wapo makini sana na tabia kama
kupanga mipango mizuri, kutumia pesa kwa busara na hata ikiwezekana
kubana matumizi ili kuhakikisha usalama wa pesa unakuwepo.
Lakini,
hata hivyo pamoja na wengi kijitahidi kufanya hivyo, bado zipo tabia
ambazo watu wanazo zinawaacha au zinasababisha wengi kuendelea kubaki
kwenye umaskini ingawa ukiangalia pia watu hao wana uwezo wa kupata pesa
kila wakati.
Kwa
hiyo hapa unaona tatizo la watu wengi sio kupata pesa, kama ni pesa
kweli wanazipata, ila shida inakuja kwa kukumbatia tabia hizo ambazo
zinawarudisha nyuma sana na matokeo yake kuwaacha katika dimbwi la
umaskini.
Leo
hapa katika makala haya, tunakuletea tabia mbaya ambazo kwa mtu yeyote
akiwa nazo ni lazima mtu huyo ataendelea kubaki kwenye umaskini. Hakuna
ujanja katika hili, kama una tabia hizi, nimesema utaendelea kubaki kuwa
maskini.



