Aenean quis facilisis massa. Cras justo odio, scelerisque nec dignissim quis, cursus a odio. Duis ut dui vel purus aliquet tristique.

Slide Title 2

Morbi quis tellus eu turpis lacinia pharetra non eget lectus. Vestibulum ante ipsum primis in faucibus orci luctus et ultrices posuere cubilia Curae; Donec.

Slide Title 3

In ornare lacus sit amet est aliquet ac tincidunt tellus semper. Pellentesque habitant morbi tristique senectus et netus et malesuada fames ac turpis egestas.

Monday, January 22, 2018

Tabia Mbaya Za Fedha Zinazowaacha Wengi Kwenye Umaskini.
Idadi kubwa ya watu linapokuja suala la pesa, wapo makini sana na  tabia kama kupanga mipango mizuri, kutumia pesa kwa busara na hata ikiwezekana kubana matumizi ili kuhakikisha usalama wa pesa unakuwepo.

Lakini, hata hivyo pamoja na wengi kijitahidi kufanya hivyo, bado zipo tabia ambazo watu wanazo zinawaacha au zinasababisha wengi kuendelea kubaki kwenye umaskini ingawa ukiangalia pia watu hao wana uwezo wa kupata pesa kila wakati.

Kwa hiyo hapa unaona tatizo la watu wengi sio kupata pesa, kama ni pesa kweli wanazipata, ila shida inakuja kwa kukumbatia tabia hizo ambazo zinawarudisha nyuma sana na matokeo yake kuwaacha katika dimbwi la umaskini.

Leo hapa katika makala haya, tunakuletea tabia mbaya ambazo kwa mtu yeyote akiwa nazo ni lazima mtu huyo ataendelea kubaki kwenye umaskini. Hakuna ujanja katika hili, kama una tabia hizi, nimesema utaendelea kubaki kuwa maskini.

Monday, March 21, 2016

MAMBO MENGINE 10 NI HAYA KUHUSU SINEMA YA TITANIC NA TUKIO HALISI..

Ikitokea Unataja Orodha ya Sinema Zenye Umarufu wake Duniani Huwezi  kuiacha Sinema ya Titanic.. Inayo Elezea kisa cha Kwelii.. Aprili10, 1912: Meli ya Titanic iliondoka Southampton, Uingereza, ikielekea New York, Marekani. Aprili 15: Saa 8:20 usiku, Titanic ilizama, watu 1,500 hivi walikufa.
sasa leo nina kupenyezea Mambo 10 yakuyajuwa kuhusu Sinema na Uhalisia wamatukio ya katika wa Meli ya Titanic!!


1.Wanamuziki waliokuwa  wakipiga muziki kwenye meli ya titanic, waliendelea kupiga muziki kwa saa moja Toka meli ilipoanza kuzama.

2.Gharama za kutengeneza Movie ya Titanic Ni Kubwa kuliko gharama za Kutengeneza Meli halisi ya Titanic iliyokuwa na uwezo wa kubeba watu zaidi ya elfu tatu! Movie ya Titanic ilitengenezwa kwa gharama ya dola Milioni miambili ($ 200Mil) wakati Meli ya Titanic ilikuwa na thamani ya $170 Mil.




3. Baada ya Kuona Meli inazama Maeneo yenye baridi kali, Mpishi Mkuu wa meli hiyo, alikunya pombe Kupita Kiasi ili aweze Kuhimili baridi Kali! Aliweza Kukaa masaa Mawili kwenye Barafu na Hatimae Kuokolewa.

4.Sekunde 30 zingetosha Kuokoa Meli ya Titanic  Kama si Kuchelewa Kutoa Taarifa za Kuwepo kwa Mwamba wa Barafu. Watoa taarifa walichelewa kwa Sekunde 30 tu!

5.Baada ya Kugongana na Mwamba, Ilipita masaa mawili mpaka Meli yote ya Titanic Kuzama.

6.Hakuna Meli Yoyote nyingine Iliyowahi Kuzama kwa kugonga Barafu!

7.Mjapani Aliyepona kwa kuokolewa Kwenye Ajali ya Titanic, aliitwa Mpumbavu nchini kwake eti tu, Kwanini hakufa kishujaa pamoja na wengine?

8. Vyumba vya Hadhi ya juu zaidi kwenye Meli ya Titanic vililipiwa Dola 200.

9. Zaidi ya Maharusi 20 walikuwa wakisherekea “HoneyMoon”  kwenye meli hiyo iliyozama.

10. Msanii Madonna ni moja kati ya watu waliotakiwa kuigiza uhusika waa “Rose” lakini baadae Kate Winslet aliigiza uhusika huo.

Monday, December 14, 2015

Ijuuwe Tuzo Maarufu zaidi Dunia...




Tuzo ya Nobel ni tuzo ya fedha kwa ajili ya mafanikio ya pekee katika fani mbalimbali. Ilianzishwa na Alfred Nobel.

Tangu mwaka wa 1901 imetolewa kwa watu waliofaulu katika fani zifuatazo: Fizikia, Kemia, Tiba (au Fiziolojia), Fasihi na Amani. Tangu mwaka wa 1969, tuzo ya sita imeongezewa kwa Uchumi. Siku hizi Tuzo ya Nobel ni tuzo ya kimataifa mashuhuri kabisa duniani. Wanaotuzwa hupokea hati, medali ya dhahabu na kiasi cha pesa cha takriban € milioni 1,2 (kinategemea mapato ya riba kutokana na mfuko wa fedha iliyotengwa kwa kusudi hii na Alfred Nobel). Maazimio kuhusu tuzo za kila mwaka hutolewa kufuatana na wasia wa Alfred Nobel na kamati zifuatazo:

Hii Ndiyo Orodha ya Maraisi wa Nchi ya Burundi..



Burundi ilundwa kama ufalme ulioongozwa na Watutsi waliotawala Wahutu. Lakini kabla ya ukoloni mipaka kati ya makundi hayo haikuwa imara mno; Wahutu matajiri katika utumishi wa mwami waliweza kupanda ngazi na kuwa Watutsi na pia Watutsi maskini waliweza kushuka ngazi na kuhesabiwa kati ya Wahutu, hasa baada ya kuoa au kuolewa na mtu wa upande mwingine. Uhusiano wa makundi hayo ulifanana zaidi na ule wa matabaka si wa makabila tofauti, pia kwa sababu lugha ilikuwa moja kwa wote.
Utawala wa kikoloni uliimarisha mipaka kati ya makundi hayo mawili maana kila mtu aliandikishwa na kupangwa katika moja kati ya makundi hayo. Pia Wabelgiji walipendelea Watutsi na kuangalia wapate nafasi zote za uchifu ambako walipaswa kutoa kibali. Kuhamia katika kundi lingine kulikwisha. Uhusiano kati ya makundi ulianza kufanana zaidi na ukabila.
Mwishoni mwa ukoloni Wabelgiji walibadilisha msimamo na kupendelea Wahutu.

Katika hali hiyo Burundi ilikaribia uhuru. Vyama vya siasa viliundwa vilivyofuata ugawaji wa kimbari kati ya Watutsi na Wahutu. Mapigano ya kwanza kati ya Wahutu na Watutsi yalitokea mwaka 1959 kabla ya uhuru yakakomeshwa na Wabelgiji.
Baada ya uhuru katika Burundi, kinyume na Rwanda, utawala ulibaki upande wa Watutsi kwa sababu jeshi lilikuwa mikononi mwao. Vipindi vya mashambulio kati ya vikundi vilifuata.