Monday, January 22, 2018

Tabia Mbaya Za Fedha Zinazowaacha Wengi Kwenye Umaskini.
Idadi kubwa ya watu linapokuja suala la pesa, wapo makini sana na  tabia kama kupanga mipango mizuri, kutumia pesa kwa busara na hata ikiwezekana kubana matumizi ili kuhakikisha usalama wa pesa unakuwepo.

Lakini, hata hivyo pamoja na wengi kijitahidi kufanya hivyo, bado zipo tabia ambazo watu wanazo zinawaacha au zinasababisha wengi kuendelea kubaki kwenye umaskini ingawa ukiangalia pia watu hao wana uwezo wa kupata pesa kila wakati.

Kwa hiyo hapa unaona tatizo la watu wengi sio kupata pesa, kama ni pesa kweli wanazipata, ila shida inakuja kwa kukumbatia tabia hizo ambazo zinawarudisha nyuma sana na matokeo yake kuwaacha katika dimbwi la umaskini.

Leo hapa katika makala haya, tunakuletea tabia mbaya ambazo kwa mtu yeyote akiwa nazo ni lazima mtu huyo ataendelea kubaki kwenye umaskini. Hakuna ujanja katika hili, kama una tabia hizi, nimesema utaendelea kubaki kuwa maskini.